HAYA NDIYO YALIYOJIRI KATIKA AJALI YA BASI HUKO SHINYANGA!!! JIONEEE HAPA!


Katika ajali hiyo ya jana, watu tisa walifariki dunia papo hapo na mmoja akifia hospitalini baada ya basi walilokuwa wakisafiria kutoka jijini Mwanza kwenda Tabora kugongana na tela la lori la kampuni ya Coca - Cola katika kijiji cha Samuye, Shinyanga Vijijini.
Ajali hiyo ilitokea jana saa 8:45 mchana katika kijiji hicho, baada ya basi la kampuni ya Unique namba T148 BKK aina ya Scania kukutana uso kwa uso na tela hilo lenye namba T635 AJT katika barabara kuu ya Shinyanga - Nzega.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Justus Kamugisha, alisema ajali hiyo ilitokana na lori la kampuni ya Coca - Cola lililokuwa na tela kulipita gari lingine, lakini kabla tela halijaingia katika barabara yake, lilikutana na basi hilo lililokuwa katika mwendo kasi na kusababisha ajali hiyo.
MFULULIZO WA AJALI
Aprili 10, 2015, watu 12 walifariki dunia katika ajali iliyohusisha mabasi matatu na gari dogo iliyotokea katika eneo la Mbwewe, Handeni, mkoani Tanga na Kikwaza, wilayani Mikuni, Morogoro.
Aprili 12, 2015, watu 18 waliteketea kwa moto baada ya basi la Kampuni ya Nganga kugongana na lori katika kijiji cha Msimba, Mikuni kwenye barabara kuu ya Morogoro – Iringa.
Aprili 17, 2015, watu 19 walifariki dunia baada ya basi dogo la abiria Toyota Hiace kupinduka na kutumbukia mtoni katika eneo la Kiwira, wilayani Rungwe, Mbeya.
Nini tatizo?
Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi.
Previous
Next Post »