DAR COACH TANZANIA LIMITED WAZIDI KUPASUA ANGA!!!

Kampuni ya Dar coach (T) limited inayojishughurisha na utengenezaji wa body za mabasi nchini Tanzania, imezidi kujipatia soko  la bidhaa zake kadiri siku zinavyokwenda ndani na nje ya nchi ya Tanzania. Kampuni hiyo ambayo hadi sasa imekwishatengeneza  body aina mbalimbali ikiwa  ni pamoja na bodi ya DIAMOND,CRYSTAL, kopi ya zhong tong climber, kopi ya yutong f11 na f12 zote zikiwa na injini za scania,tata na fuso  , imezidi kupata soko  nchi za nje Kama Burundi na Rwanda kuringana na ubora wa bidhaa zake.

Taarifa kutoka katika chanzo chetu cha habari zinasema kuwa kwa sasa kampuni inapokea order nyingi kutoka nchi hizo mbili za Rwanda na Burundi ,kuringanisha  na nchi nyingine za ukanda wa afrika mashariki.

Hii ni chachu ya maendeleo kwa nchi ya Tanzania katika sekta hii ya viwanda ambayo serikali ya awamu ya tano  ilikuwa ikisisitiza sana.

Changamoto kubwa ambayo imetajwa kuwa ni kikwazo sana katika shughuli hizi, ni gharama kubwa ya kodi katika uagizaji wa malighafi zinazotumika kutengenezea bodi hizo za mabasi, kiasi cha kupelekea  uzarishaji kuwa Mdogo.

Previous
Next Post »